Mwanamuziki mashuhuri nchini
Marekani Kanye West, ambaye majuzi alilazwa hospitalini baada
ya
kutatizwa na msongo wa mawazo na uchovu, amekutana na rais mteule wa
Marekani Donald Trump jijini New York.
Bw Trump anasema wawili hao walizungumza kuhusu "maisha" kabla ya kupigwa picha pamoja.
Alisema
wawili hao ni "marafiki" na akamweleza Kanye kuwa "mtu mzuri" lakini
hakusema iwapo mwanamuziki huyo atatumbuiza wakati wa sherehe ya
kuapishwa kwake mwezi Januari.
Kanye alisalia kimya alipokuwa na mwanachama huyo wa Republican.
Aliwaambia wanahabari: "Nataka tu kupigwa picha kwa sasa."
Taarifa
kutoka Marekani zinasema Bw Trump huenda anakabiliwa na tatizo katika
kutafuta wanamuziki mashuhuri wa kutumbuiza siku ya kuapishwa kwake.
EmoticonEmoticon