JAMANI MIMBA YA JOKATE A.K.A. KIDOTI YADAIWA KUCHOROPOKA

JAMANI MIMBA YA JOKATE A.K.A. KIDOTI YADAIWA KUCHOROPOKA

Mimba ya Jokate yadaiwa kuchoropoka

Mwanamitindo maarufu Bongo, Jokate Mwegelo ‘Kidoti’

IMEFICHUKA! Ile mimba ya mwanamitindo maarufu Bongo, Jokate Mwegelo ‘Kidoti’ iliyokuwa ikisemekana ni ya Mbongo-Fleva, Ali Saleh Kiba inadaiwa kuharibika kwa kuchoropoka kisa kikiwa ni mazoezi makali aliyoyafanya hivi karibuni.

Kidoti na Ali Kiba

Chanzo makini kililiambia gazeti hili kwamba, Jokate kwa sasa hana ujauzito tena kwani ulichoropoka kufuatia mazoezi makali ya kujiandaa na shoo aliyofanya ya Nyama Choma Festival kwenye Viwanja vya Leaders Club Kinondoni jijini Dar iliyosapotiwa na mpenzi wake huyo.


“Kama mlikuwa hamjui kitumbo cha Jojo (Jokate) kilichoropoka kutokana na mazoezi makali ya shoo aliyoifanya hivi karibuni ambapo kwa sasa anaendelea vizuri na anafanya kazi zake kama kawaida bila ujauzito,” kilinyetisha chanzo hicho.

Baada ya kupata habari hizo, paparazi wetu alimtafuta Jokate na kumuuliza kuhusu ujauzito wake ambapo alijibu kwa ufupi: “Kwa sasa mimi sina mimba.”

Hata hivyo, chanzo hicho kiliendelea kueleza kwamba, kwa sasa Kiba anajipanga upya katika masuala hayo ya


WEMA SEPETU AMPIGIA SALUTI DIAMOND KWA WIMBO WAKE MPYA WA UTANIPENDA

WEMA SEPETU AMPIGIA SALUTI DIAMOND KWA WIMBO WAKE MPYA WA UTANIPENDA


Wema ampigia saluti Diamond

Wema Sepetu ‘Madam’

MTOTO mzuri Bongo Movies, Wema Sepetu ‘Madam’ ameonesha kumpigia saluti mpenzi wake wa zamani, Nasibu Abdul ‘Diamond’ baada ya kuguswa na ubora wa wimbo wake mpya uitwao Utanipenda kwa kuposti video mtandaoni ikimuonesha akiuimba wimbo huo.

Nasibu Abdul ‘Diamond’.

Kwenye video hiyo, Madam anaonekana akiwa na shosti wake mwigizaji Aunt Ezekiel wakiimba wimbo huo kwa staili ya kupokezana huku wakiwa wamejilaza kitandani.


Mmoja wa marafiki wa Madam aliyeiona video hiyo, alisema zilipendwa huyo wa Diamond amejirekodi video hiyo kwani ameukubali na unagusa hisia za kila mtu ndiyo maana akajikuta amejirekodi na kuutupia katika Mtandao wa Instagram bila kujali kwamba walishamwagana.

Alipotafutwa Madam kuhusiana na ishu hiyo, alisema amejirekodi video hiyo kwani ameikubali na amekuwa akipenda sana nyimbo za Diamond hata kabla hawajawa na uhusiano na isitafsiriwe kwamba anataka kurejesha majeshi.

“Nilipenda nyimbo zake hata kabla hatujawa kwenye uhusiano na mimi nitaendelea kuwa shabiki wa nyimbo zake siku zote, mapenzi yalishakufa,” alisema Madam.



MTANGAZAJI MAARUFU PENNY AFANYA NYUMBANI KWAKE KAMA CLABU NDOGO

MTANGAZAJI MAARUFU PENNY AFANYA NYUMBANI KWAKE KAMA CLABU NDOGO



Penny Mungilwa Nyumbani kwake kuna klabu ndogo

Mtangazaji Penniel Mungilwa ‘Penny’.

SIKU zote hapa huwa tunawatembelea mastaa mbalimbali nyumbani kwao. Leo tunaye Mtangazaji Penniel Mungilwa ‘Penny’ anayeishi maeneo ya Mwananyamala jijini Dar.

Anaipenda nyumba yake. Ameidizaini mapambo kwani mwenyewe pia anafanya shughuli hiyo na kutengeneza kipato pia. Mbali na kupambwa na vitu tofauti, nyumbani kwake kuna klabu ndogo yenye vinywaji vilivyo na kilevi na vya kwaida.


Kama hiyo haitoshi, kuna  eneo maalum aliloweka mtungi wa shisha. Anatumia sanjari na marafiki zake wanaotumia kilevi hicho pale wanapomtembelea.

Source;Global


MKULIMA WA BANGI  ANASWA HUKO SONGEA

MKULIMA WA BANGI ANASWA HUKO SONGEA

Mkulima wa bangi anaswa

Mtuhumiwa akiwa chini ya ulinzi na pingu mkononi wakati askari aking’oa bangi hizo shambani.

KIBANO! Jeshi la Polisi Mkoa wa Ruvuma limemnasa mkulima mmoja, Kiliani Fussi (pichani) kwa tuhuma za kulima bangi kwa kificho kwenye shamba lake maalum huku akijua ni kosa kisheria, twende na Risasi Jumamosi.

Polisi wakijadiliana jambo

Zoezi hilo lilifanyika hivi karibuni ambapo mkulima huyo alishtukizwa na askari akiwa kwenye shamba hilo lenye ukubwa wa nusu eka ambalo lipo kwenye Mtaa wa Namanyigu katikati ya Manispaa ya Mji wa Songea.

…wakiichoma moto bangi hiyo

Polisi wakiongozwa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma, Mihayo Msikhela na Afisa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Mkoa, Revacus Malimi walilifikia shamba hilo kwa tabu kwani njia ya kuelekea ilikuwa ina majani aina ya upupu ambayo yana sifa ya kuwasha hali iliyowalazimu polisi hao kuyafyeka kwanza majani hayo ili kuweza kupita kwa urahisi.

Polisi wakifanya ukaguzi shambani humo.


Baadhi ya mashuhuda wa tukio hilo kwa nyakati tofauti  waliliambia Risasi Jumamosi kwamba, Fussi amekuwa  mkulima wa siku nyingi wa mmea huo haramu lakini huwa analindwa na baadhi ya viongozi licha ya raia wema kutoa taarifa.

Walisema kuwa, majirani wenzake ambao wanalima katika eneo moja mazao ya chakula na biashara walijaribu kumuonya kuhusu ulimaji wa zao hilo, lakini hakuwasikiliza.

Kama kawaida yake, Risasi Jumamosi lilimdaka Kamanda Msikhela ili aweze kuzungumzia sakata hilo la ukomeshaji wa kilimo haramu cha bangi nchini ambacho kimekuwa kikileta madhara makubwa kwa jamii ambapo alisema:

Shamba la bangi

“Jeshi la polisi lilifanikiwa kukamata shamba hilo la bangi baada ya kupokea taarifa kutoka kwa raia wema. Mtuhumiwa tumemkamata na taratibu za kisheria zinaendelea ili afikishwe mahakamani.”

Kamanda Msikhela aliwataka wananchi, kuendelea kutoa taarifa za siri kwa jeshi la polisi punde wanapobaini kuwepo kwa uvunjwaji wa sheria za nchi katika maeneo yao.

Source;Global


Tishio la 'Bomu' lalazimu ndege ya Ufaransa kutua Kenya

Wataalamu hao wanatoka kikosi cha jeshi la wanamaji wa Kenya na idara ya polisi wa upelelezi. Ndege moja ya abiria ya Air France Boeing 777 AF463, inayohudumu kati ya Mauritius na Paris imelazimika kutua kwa ghafla katika uwanja wa ndege wa kimataifa mjini Mombasa - Kenya baada ya kifaa kinachodhaniwa kuwa bomu kupatikana ndani ya choo cha ndege hiyo.
Mhudumu mmoja wa ndege hiyo alimfahamisha rubani kuhusiana na kifaa hicho ndipo shughuli za kutua kwa dharura zikaanza. Katika mtandao wake wa kijamii wa Twitter, kamanda mkuu wa polisi nchini Kenya Jenerali Joseph Boinnet, amesema kuwa ndege hiyo iliyokuwa njiani kuelekea Paris Ufaransa ikiwa na abiria 473 na wahudumu 14 ilitua salama na abiria wote kuokolewa. Image copyright Reuters Image caption 'Bomu' yasababisha ndege ya Ufaransa kutua Kenya Ndege hiyo inasemekana kutua saa sita usiku wa kuamkia leo Jumapili, huku wataalamu wa kutegua mabomu kutoka jeshila wanamaji la Kenya wakiingia ndani ya ndege hiyo kukagua kifurushi kilicholeta taharuki. Habari za hivi punde zinasema kuwa maafisa wa upelelezi wanasemekana kuwa wamewatambua washukiwa wawili abiria wa ndege hiyo. Shirika linalosimamia viwanja vya ndege nchini Kenya linasema kuwa kifaa hicho kimeondolewa ndani ya ndege hiyo. Shughuli za kawaida za usafiri zimerejea katika uwanja huo wa ndege baada ya kusitishwa ilikukabiliana na tishio hilo.

Kategori

Kategori