Papa Francis kutua kenya na ujumbe wa amani

Papa kutua Kenya Kesho.




Nairobi, Kenya. Kiongozi wa Kanisa Katoliki Papa Francis amesema kwamba kesho akiwa Kenya atatoa ujumbe wa amani.
Kiongozi huyo Katika taarifa aliyoituma juzi, alitoa wito kwa waandaaji wa ziara yake wakumbuke kuomba ili

ziara hiyo ilete matumaini kila mmoja.
Utafiti uliofanywa na kampuni ya Infotrak mwishoni mwa wiki ulionyesha kuwa asilimia 93 ya raia wa Kenya wana hamu ya ziara ya kiongozi huyo wa kanisa Katoliki ulimwenguni.
“Wakenya wengi wanatarajia kujitokeza mapokezi ziara ya Papa kesho. Matarajio hayo yako kwa Wakenya wote bila kujali dini wala kabila,” alisema Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Infotrak Angela Ambitho.
Alisema raia wa nchi hiyo 777 walihusishwa katika utafiti huo uliofanywa Ijumaa. Asilimia 98 ya Wakatoliki wanafurahia ziara ya Papa Francis na asilimia 91 ya Wakenya wa madhehebu na dini zingine walisema wanamkaribisha Kenya.
Utafiti huo ulionyesha kuwa Papa Francis anayefanya ziara yake ya kwanza Afrika anapendwa na Wakenya wote Wakatoliki na wasio Wakatoliki.
“Papa Francis anapendwa na Wakatoliki ambao wamekumbatia unyenyekevu wake na wito wa kushirikisha wote,” alisema Ambitho.
“Kupendwa kwa Papa kunaonekana kupiku Kanisa Katoliki ambalo licha ya kukumbwa na kashfa mbalimbali ulimwenguni lina wafuasi wengi Kenya,” aliongeza

Mabadiliko
Kwa mujibu wa utafiti huo, asilimia 95 ya Wakatoliki nchini Kenya wanahisi Papa Francis ataleta mabadiliko katika kanisa hilo.
Aidha, asilimia 98 ya Wakatoliki Kenya wanahisi kwamba Papa Francis ataleta mabadiliko mazuri katika dini ya Kikristo, asilimia 85 ya Wakenya wa madhehebu mengine wanahisi kwamba ataleta mabadiliko katika dini


EmoticonEmoticon