Njaaaa

Njaaaa


Mastaa:imezua jambo! Kufuatia tumbuatumbua inayoendeshwa na Rais Dk. John Pombe Magufuli kwa vigogo waliokuwa wanawapa jeuri mastaa wa kike mjini, wenyewe wameibuka na kusema kiongozi huyo ‘amewaua’ kwa njaa.

Chanzo makini kililiambia gazeti hili kuwa mastaa wengi wa kike wanalalamika njaa na ndiyo maana tangu alipoingia madarakani Rais Magufuli na kuanza kuwaondoa mafisadi, wasanii hao wamekuwa hawaonekani viwanja kama zamani kwa sababu hawana mkwanja.

“Yaani wasanii wa kike wana hali mbaya sana ndiyo maana hamuoni wakiwa na mbwembwe kama zamani wamekuwa wakijifungia ndani tu hawataki kuonana na watu kwani hata hela za kwenda saluni kujiremba hamna maana wanasema waliokuwa wakiwapa jeuri wengi wao wamekumbwa na tumbua majipu,” kilisema chanzo hicho.

Baada ya kupata ubuyu huo, paparazi wetu aliwatafuta baadhi ya mastaa ambapo walikuwa na haya ya kusema;

ISABELA MPANDA

“Kweli tumeathirika sana na hii tumbua majipu maana waliokuwa wakitupa fedha nyingi hata ukiomba milioni wanatoa kwa sasa wanaogopa hata ukiwapigia simu hawapokei huku wengine wakiwa ni wale vigogo waliokamatwa, Rais Magufuli ametunyoosha.”

BABY MADAHA

“Kiukweli lazima iathiri kwa sababu ilikuwa rahisi kwa mtu kudhamini hata katika muvi. Kipindi cha Kikwete (Jakaya, Rais wa awamu ya nne) mtu anakupa milioni 20 au 30 kwenye muvi lakini sasa hivi, thubutu.”


MIRIAMU JOLWA ‘JINI KABULA’

“Mimi sina kawaida ya kutoka na mapedeshee, bwana’ngu ni wa kawaida sana kwa hiyo sijui kama imeathiri vipi hiyo tumbua majipu.”

Source;Global




Wastara amsifia  yusufu mlela kwa utendaji wa kazi  amfananisha na sajuki kwa baadhi ya mambo

Wastara amsifia yusufu mlela kwa utendaji wa kazi amfananisha na sajuki kwa baadhi ya mambo

Wastara: Huyu Jamaa Nampenda Mfano Hakuna, Anafanana Vingi na Sajuki
Mama na mwana mama na baba nimeipenda kama ilivyo ila kiukweli huyu jamaa nampenda mfano hakuna, mpole muelewa hana makuu anao ubinadaamu hana ugomvi na mtu, mpole ajui kufoka wala kugombana akikasirika dk 2 tu anarudi kuwa normal. Sichoki kufanya nae kazi namchukulia ni mdogo wangu wa tumbo moja namfananisha vitu vingi na Sajuki si mwingine ni      Yusuph Mlela au Mlelandro.
Hayo ni maneno ya mwigizaji Wastara Juma kwenye moja ya post zake kwenye mtandao picha wa instagram mara baada ya kuweka picha hiyo hapo juu akiwa Yusuph Mlela.
Je wajua kuwa staa kwa kibongo  Diamond alikuwa uso kwa uso na watoto wengine wa zari? Tazama picha hizi

Je wajua kuwa staa kwa kibongo Diamond alikuwa uso kwa uso na watoto wengine wa zari? Tazama picha hizi

DIAMOND PLATNUMZ USO KWA USO NA WATOTO WA ZARI TAZAMA HAPA 
tazama picha upate kujua undani wa familia ya mwamuziki wa bongo flava anayetamba na wimbo wake mpya wa UTANIPENDA
Hatimaye Diamond amekutana na familia ya mpenzi wake, Zarinah hassan.
Diamond ambaye alikua nchini Uganda kwa ajili ya show ya ‘Born To Win’ amepata nafasi ya kukutana na watoto wengine watatu wa Zari.
Diamond aliweka picha akiwa na Familia ya zari na kuandika “Me and my Stars!…Basi Hapo Vikurubembe roho zinawau
                        Diamond, Tiffah na mama mzazi wa Zari.

Jamani mchungaji asweka jela mwaka 1 kwa kosa la wizi

Mchungaji kiongozi KKKT jela kwa wizi
Mchungaji kiongozi wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Rauya, Zawadiel Maruchu amehukumiwa kifungo cha

PICHA ZA WEMA SEPETU NA RAY ZALETA GUMZO MITANDAONI

SUPER STAR WEMA SEPETU NA RAY WATUPIA PICHA ILIYOZUA GUMZO MTANDAONI

Perfect blog







USIPITWE NA MAGAZETI YA LEO SOMA HABARI ZILIZOTIKISA UJIONEE

December 25, 2015Magazeti ya Tanzania December 25 2015 na stori zake kubwa kurasa za mwanzo na mwisho

Usikose na usipitwe na magazeti ya Leo 25 2015 nimekuwekea tena stori zote kubwa za Magazeti ya Tanzania kuanzia kwenye Udaku, michezo na hardnews ili ujue kinachoendelea mtu wangu,






.
.
.
.
.
.

WAJUE WASANII WA KIKE WENYE MASHABIKI WENGI SOKONI KWA SASA

WASANII WA KIKE WENYE MASHABIKI WENGI SOKONI



Staa wa sinema za Kibongo, Jenifer Kyaka 'Odama' 

Hawa ni miongoni mwa wasanii watatu wa kike, ambao wanafanya vizuri katika tasnia ya filamu hapa nchini Tanzania kwa utengenezaji bora wa filamu hizo na zenye kuvutia mashabiki hasa katika uuzwaji wa filamu zao hii inawafanya waendelee kuwa bora kila mwaka katika soko la filamu kutokana na ubunifu na mbinu mbalimbali katika utengenezwaji wa filamu zao .

Msanii wa Filamu za Bongo, Riyama Ally

Wasanii hawa wamejizolea umahiri huo kutoka kwa mashabiki wao kwa kuwavuta kihisia kutokana na madhari wanazokuwa wakifanyia filamu zao.

Hii imedhiilika mwaka huu kwani hawana tatizo na watu kwani wao wanawaza kufanya kazi zao kiufanisi zaidi.

Msanii wa Filamu za Bongo, Shamsa Ford

JAMANI MIMBA YA JOKATE A.K.A. KIDOTI YADAIWA KUCHOROPOKA

JAMANI MIMBA YA JOKATE A.K.A. KIDOTI YADAIWA KUCHOROPOKA

Mimba ya Jokate yadaiwa kuchoropoka

Mwanamitindo maarufu Bongo, Jokate Mwegelo ‘Kidoti’

IMEFICHUKA! Ile mimba ya mwanamitindo maarufu Bongo, Jokate Mwegelo ‘Kidoti’ iliyokuwa ikisemekana ni ya Mbongo-Fleva, Ali Saleh Kiba inadaiwa kuharibika kwa kuchoropoka kisa kikiwa ni mazoezi makali aliyoyafanya hivi karibuni.

Kidoti na Ali Kiba

Chanzo makini kililiambia gazeti hili kwamba, Jokate kwa sasa hana ujauzito tena kwani ulichoropoka kufuatia mazoezi makali ya kujiandaa na shoo aliyofanya ya Nyama Choma Festival kwenye Viwanja vya Leaders Club Kinondoni jijini Dar iliyosapotiwa na mpenzi wake huyo.


“Kama mlikuwa hamjui kitumbo cha Jojo (Jokate) kilichoropoka kutokana na mazoezi makali ya shoo aliyoifanya hivi karibuni ambapo kwa sasa anaendelea vizuri na anafanya kazi zake kama kawaida bila ujauzito,” kilinyetisha chanzo hicho.

Baada ya kupata habari hizo, paparazi wetu alimtafuta Jokate na kumuuliza kuhusu ujauzito wake ambapo alijibu kwa ufupi: “Kwa sasa mimi sina mimba.”

Hata hivyo, chanzo hicho kiliendelea kueleza kwamba, kwa sasa Kiba anajipanga upya katika masuala hayo ya


WEMA SEPETU AMPIGIA SALUTI DIAMOND KWA WIMBO WAKE MPYA WA UTANIPENDA

WEMA SEPETU AMPIGIA SALUTI DIAMOND KWA WIMBO WAKE MPYA WA UTANIPENDA


Wema ampigia saluti Diamond

Wema Sepetu ‘Madam’

MTOTO mzuri Bongo Movies, Wema Sepetu ‘Madam’ ameonesha kumpigia saluti mpenzi wake wa zamani, Nasibu Abdul ‘Diamond’ baada ya kuguswa na ubora wa wimbo wake mpya uitwao Utanipenda kwa kuposti video mtandaoni ikimuonesha akiuimba wimbo huo.

Nasibu Abdul ‘Diamond’.

Kwenye video hiyo, Madam anaonekana akiwa na shosti wake mwigizaji Aunt Ezekiel wakiimba wimbo huo kwa staili ya kupokezana huku wakiwa wamejilaza kitandani.


Mmoja wa marafiki wa Madam aliyeiona video hiyo, alisema zilipendwa huyo wa Diamond amejirekodi video hiyo kwani ameukubali na unagusa hisia za kila mtu ndiyo maana akajikuta amejirekodi na kuutupia katika Mtandao wa Instagram bila kujali kwamba walishamwagana.

Alipotafutwa Madam kuhusiana na ishu hiyo, alisema amejirekodi video hiyo kwani ameikubali na amekuwa akipenda sana nyimbo za Diamond hata kabla hawajawa na uhusiano na isitafsiriwe kwamba anataka kurejesha majeshi.

“Nilipenda nyimbo zake hata kabla hatujawa kwenye uhusiano na mimi nitaendelea kuwa shabiki wa nyimbo zake siku zote, mapenzi yalishakufa,” alisema Madam.



MTANGAZAJI MAARUFU PENNY AFANYA NYUMBANI KWAKE KAMA CLABU NDOGO

MTANGAZAJI MAARUFU PENNY AFANYA NYUMBANI KWAKE KAMA CLABU NDOGO



Penny Mungilwa Nyumbani kwake kuna klabu ndogo

Mtangazaji Penniel Mungilwa ‘Penny’.

SIKU zote hapa huwa tunawatembelea mastaa mbalimbali nyumbani kwao. Leo tunaye Mtangazaji Penniel Mungilwa ‘Penny’ anayeishi maeneo ya Mwananyamala jijini Dar.

Anaipenda nyumba yake. Ameidizaini mapambo kwani mwenyewe pia anafanya shughuli hiyo na kutengeneza kipato pia. Mbali na kupambwa na vitu tofauti, nyumbani kwake kuna klabu ndogo yenye vinywaji vilivyo na kilevi na vya kwaida.


Kama hiyo haitoshi, kuna  eneo maalum aliloweka mtungi wa shisha. Anatumia sanjari na marafiki zake wanaotumia kilevi hicho pale wanapomtembelea.

Source;Global


Kategori

Kategori